11 Novemba 2014 - 04:07
Ujerumani: hali Mashariki mwa Ukraine haiko sawa

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier amesema hali katika maeneo yanayoshikiliwa na waasi, Ukraine imeanza tena kuwa tete na pande zote zinapaswa kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano.

Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier amesema hali katika maeneo yanayoshikiliwa na waasi, Ukraine imeanza tena kuwa tete na pande zote zinapaswa kuheshimu makubaliano ya kusitisha mapigano.
Tamko la Waziri Frank-Walter Steinmeier alilolitoa wakati akiwa ziarani nchini Kazakhstan, lilionesha wasiwasi wake kufuatia ongezeko la mapigano mjini Donetsk na Luhansk kati ya vikosi vya serikali na waasi wanaotaka kujitenga wanaoiunga mkono Urusi.
Hali hii imetoakea licha ya kuwepo makubaliano ya kusitisha mapigano yaliotiwa saini katika mji mkuu wa Belarus, Minsk tarehe tano Septemba.
"Kwa bahati mbaya, hali imerejea tena kuwa tete sasa nafikiri tunapaswa kuwaita wale wote wanaousika na mgogoro huu, pamoja na upande wa Urusi kurejea kuangalia tena makubaliano ya Minsk," alisema Steinmeier katika mkutano na waandishi habari.
Waziri huyo wa mambo ya nchi za nje wa Ujerumani ameongeza kuwa atakaporejea mjini Berlin hii leo jioni atajadili hali ya Ukraine na Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Federica Mogherini.
Aidha eneo la Donetsk Mashariki mwa Ukraine lilishuhudia mapigano makali siku ya Jumapili huku shirika la Usalama na Ushirikiano la Ulaya OSCE likisema limeona magari ya kijeshi yasiokuwa na nembo yoyote, katika maeneo ya waasi ambapo Ukraine kupitia msemaji wa baraza la usalama wa Kitaifa Andriy Lysenko, inaamini kuwa Urusi ndio iliyotuma jeshi lake huko.
"Katika eneo la Makiivka mjini Donetsk unaodhibitiwa na waasi kulionekana msururu wa magari 40, baadhi yao yakiwa na silaha nzito, Hasa makombora. Pia waangalizi wa shirika la usalama na ushirikiano la Ulaya waliwaona wanajeshi waliovalia sare ya kijivu bila ya utambulisho wowote," alisema Andriy Lysenko.

Lebo